Tuesday, July 26, 2016

SERENGETI BOYS KAMBINI MADAGASSAR


 

 
Na Tausi Salum
DUAza Watanzania zielekezwe pia kwa timu ya Taifa ya Mpira 

wa Miguu ya vijana wenye umri wa chini ya miaka 17 ‘Serengeti 

Boys’, iliyoondoka leo saa 12.00 Uwanja wa Ndege ya Mwalimu 

Julius K. Nyerere, Dar es Salaam, Tanzania kwenda Antananarivo, 

Madagascar kupitia Uwanja wa Ndege wa Ndege ya Oliver Tambo 

jijini Johannesburg, Afrika Kusini.

Ofisa Habari wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) 

Alfred Lucas, alisema Serengeti Boys inayokwenda kuweka kambi 

huko Antananarivo, Madagascar inatarajiwa kufika huko saa 8.10 

mchana. Timu hiyo inajiandaa kucheza na Afrika Kusini katika 

mchezo wa awali kuwania nafasi ya kucheza fainali za Kombe la 

Mataifa ya Afrika utakaofanyika Agosti 6, 2016.

Alisema mchezo wa marudiano utafanyika Agosti 21, mwaka huu 

kwenye Uwanja wa Azam, ulioko Chamazi-Mbagala, nje kidogo ya 

jiji la Dar es Salaam. Serengeti ipo kwenye ushindani wa kuwania 

nafasi ya kufuzu fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa vijana, 

zitakazofanyika mwakani huko Madagascar.

Wakati mkuu wa msafara akiwa ni Ayoub Shaibu Nyenzi ambaye 

ni Mwenyekiti wa Kamati ya Soka la Vijana, maofisa wengine 

waliosafiri na timu hiyo ni Kocha Mkuu, Bakari Nyundo Shime, 

Daktari wa timu hiyo, Shecky Francis Mngazija na Mtunza Vifaa, 

Andrew Vanance Andrew pamoja na Juma Kaseja Juma ambaye 

kwa muda amechukua nafasi ya makocha wasaidizi, Sebastian 

Nkoma na Muharam Mohammed ‘Shilton’ wanaohudhuria kozi ya 

makocha ngazi ya juu inayoratibiwa na CAF.

Nyota waliosafiri ni pamoja na makipa, Ramadhani Awm Kabwili,

Kelvin Deogratius Kayego na Samwel Edward Brazio wakati 

mabeki wako Kibwana Ally Shomari, Nickson Clement Kibabage, 

Israel Patrick Mwenda, Dickson Nickson Job, Ally Hussein 

Msengi, Issa Abdi Makamba na Enrick Vitalis Nkosi.

Viungo ni Kelvin Nashon Naftal, Ally Hamisi Ng’anzi, Asadi Ali 

Juma Ali, Syprian Benedictor Mtesigwa, Ibrahim Abdallah Ali, 

Shaban Zuberi Ada huku washambuliaji wakiwa ni Mohammed 

Abdallah Rashid, Yohana Oscar Mkomola na Muhsin Malima 

Makame.

“Najua mchezo utakuwa mgumu, lakini nakiamini kikosi change. 

Kiko imara,” amesema Shime, maarufu zaidi kwa jina la Mchawi 

Mweusi.

Serengeti Boys inakwenda kucheza na Afrika Kusini baada ya 

kuwatoa Shelisheli kwa jumla ya mabao 9-0 katika mechi zake 

mbili za kimataifa. Mshindi wa jumla kati ya Serengeti Boys na 

Afrika Kusini, atacheza na timu mshindi kati ya Namibia na 

Congo-Brazaville.

 Hivi karibuni Serengeti Boys ilifanya ziara India ambako 

walishiriki mashindano ya vijana ya Kimataifa yanayotambuliwa na 

FIFA (AIFF International Youth Tournament 2016) kabla ya 

kurudi na rekodi ya kupigiwa mfano si tu katika Tanzania na kwa 

nchi za Afrika Mashariki. Ilishika nafasi ya tutu nyuma ya Korea 

Kusini na Marekani.
mwisho
 
 

No comments:

Post a Comment