Sunday, July 31, 2016

SIMBA YAKUBALI KUBADILISHA MFUMO WA UENDESHAJI

Uongozi wa Simba Sc leo umekubali rasmi kubadili mfumo wa uendeshaji wa klabu hiyo.

Hatua hiyo imekuja katika mkutano mkuu leo ikiwa siku chache baada ya mfanyabiashara Mohamed Dewji Mo kutoka hadharani na kutaka kuwekeza kiasi cha bilioni 20.

Kufuatia hatua hiyo..sasa ni wazi kuwa kamati ya utendaji ya klabu hiyo inabidi ikutane ili itengeneze mfumo rasmi wa hisa wa uendeshaji wa klabu hiyo.

WANACHAMA WACHARUKA SIMBA SC

Simba wamepania kufanya mabadiliko katika mfumo wa uendeshaji, leo wamesikika wakifanya mabadiliko ya kauli mbiu yao ya 'Simba Nguvu Moja' na kuwa 'Simba Mabadiliko'.

Hayo yametokea asubuhi hii kwenye mkutano mkuu baada ya Rais wa klabu hiyo Evance Aveva kusimama ili kufungua mkutano huo ndipo aliposema 'Simba' akitarajia kujibiwa 'Nguvu Moja' katika hali ya kushangaza wanachama hao walijibu kwa pamoja 'Mabadiliko'.


Kabla ya hapo wanachama hao walilipuka kwa furaha pale iliposomwa ajenda ya tisa inayozungumzia maboresho ya mfumo wa uendeshaji huku ikionyesha wazi wanahitaji mabadiliko ya kuondoka kwenye mfumo wa Uanachama na kwenda kwenye Hisa.

Tayari mfanyabiashara Mohamed Dewji 'Mo' ameshaweka wazi nia yake ya kutaka kuwekeza katika klabu hiyo kwa kutoa kiasi Sh 20 Bilioni.

31Jul2016

Saturday, July 30, 2016

MO AIBUKIA MAZOEZINI SIMBA SC



Mfanyabishara kijana na maarufu ndani na nje ya nchi, Mohammed Dewji ‘MO’ ambaye ametajwa kutaka kuwekeza kwenye Klabu ya Simba kwa kutoa Sh bilioni 20, jana aliibuka kwenye mchezo wa kirafiki wa timu hiyo dhidi ya Moro Kids.

Katika mchezo huo uliochezwa kwenye Uwanja wa Chuo cha Biblia Highlands, Morogoro uliishuhudia Simba ikishinda mabao 2-0 dhidi ya wenyeji hao na kuwa ushindi wa pili mfululizo baada ya wiki iliyopita kuifunga Polisi Moro mabao 6-0.

Mabao ya Simba yalifungwa na Ibrahim Ajib dakika ya 20 akipokea pasi ya Shiza Kichuya na la pili lilifungwa na Danny Lyanga dakika ya 69 akiunganisha pasi ya Mohammed Ibrahim.

Katika hali isiyokuwa ya kawaida, mashabiki waliojitokeza uwanjani hapa muda wote wa mchezo walikuwa wakiimba nyimbo za kuushinikiza uongozi umpe timu MO.
Mashabiki hao walisikika wakiimba: “Mo tumpe timu.”


Baada ya mchezo huo Kocha Joseph Omog wa Simba alisema, amefurahishwa na uwezo ulioonyesha na wachezaji wake huku akidai wapinzania wao walikuwa katika kiwango bora zaidi

Friday, July 29, 2016

MWADINI,KIMWAGA WATOLEWA KWA MKOPO AZAM FC


UONGOZI wa klabu ya Azam FC, umeweka wazi kuwatoa wachezaji wake wanne kwa mkopo ambao ni  Mwadini Ali, Ame Ali ‘Zungu’ Abdallah Khery na Joseph Kimwaga.

Akizungumza na Jambo Leo, Makamu Mwenyekiti wa klabu hiyo Idrissa Nassor, alisema kuwa wachezaji hao ambao bado wana mikataba katika klabu yao, wameamua kuwapa nafasi za kucheza kupitia klabu za African Lyon, Simba na Mwadui FC.

Nassor alisema Mwadin Ali na Ame Ali wataichezea Simba, kwa sasa wanaendelea kufuata utaratibu wa uhamisho huo wa mkopo, Kimwaga ataitumikia klabu ya Mwadui FC ya mkoani Shinyanga na Kheri ataichezea klabu ya African Lyon.

Alisema kwa upande wa Mwadin na Ame wakati wowote kuanzia Jumatatu watajiunga na klabu ya Simba kwa kuwa vitu vilivyobaki kukamilisha uhamisho huo ni vidogo.

“Mwadini na Ame, Kimwaga na Kheri  wote tumewatoa kwa mkopo, lakini wakifanya vizuri katika klabu hizo hata kwenye mzunguko wa pili wa msimuu ujaoanza wanaweza kurejea katika klabi yetu, kikubwa ni kocha kiridhika na uwezo wao ambao itauonesha"alisema Nassor.

Alisema klabu hiyo katika msimu uliopita ilimtoa kwa mkopo mchezaji wake kwa mkopo  katika klabu ya Mwadui na mwaka huu mchezaji huyo amerejea katika kikosi cha Azam na anaitumikia.

Wakati huo huo klabu ya Azam FC leo itajitupa kwenye Uwanja wa Amaan visiwani Zanzibar kuvaana na timu ya Jang'ombe, mchezo wa kirafiki wa kijipima nguvu ikiwa sehemu ya kujiandaa na mchezo wa ngao ya jamii utakaofanyika Agosti 17 dhidi ya Yanga.

Nassor alisema kuwa mchezo huo utacheza saa 2.usiku ambapo utakuwa ni mchezo wa pili baada ya kucheza mchezo wa kwanza dhidi ya kombaini ya Zanzibar,


KARIA ATETA NA WAAMUZI

M
AKAMU wa Rais katika Shirikisho la Mpira wa Miguu (TFF), Wallace Karia amewaagiza waamuzi wenye Beji kutoka Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) kadhalika waamuzi waandamizi waliohitimu kozi leo Julai 29, 2016 kutokuwa wachoyo wa kutoa elimu waliyopata kwa wenzao wa madaraja ya kwanza, pili na tatu.

Karia aliyefunga kozi hiyo na kugawa vyeti kutoka FIFA kwa wahitimu 48, alisema hayo jana kwenye Ukumbi wa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam wakati wa hafla ya kufunga kozi hiyo iliyochukua takribani siku tano ambako sehemu ya mafunzo hayo ilikuwa ni kusoma baadhi ya marekebisho kwa msimu wa 2016/17.


“Tuna matagemeo makubwa kutoka kwenu, lakini nasema mfikirie kusaidia wenzenu ili kama si kumaliza matatizo kwenye soka basi yapungue, nasisitiza msiwe wachoyo, fundisheni wengine na muwape hamasa,” alisema Karia kwa niaba ya Rais Jamal Malinzi ambaye kwa sababu za majukumu, hakudhuria hafla hiyo.

Karia ambaye aliishukuru FIFA kuendelea kutoa kozi nyingi nchini, alisema kwamba tayari Tanzania imefaidika kwa kozi za makocha na makamishna, lakini akaagiza Idara ya Ufundi ya TFF chini ya Kocha Mkongwe, Salum Madadi kutoa mafunzo hayo kwa viongozi wa klabu na waandishi wa habari ambao ni sehemu kubwa ya familia ya mpira wa miguu.

Alisema kwamba umahiri wa makocha utakuwa chachu ya mafanikio ya soka la Tanzania kwa kutoa waamuzi bora watakaokuwa wakipata nafasi kubwa ya kuchezesha michezo mbalimbali ya mpira wa miguu.

“Mkifanya vibaya kwenye mashindano, mtakuwa mmejiharibia wenyewe na pia kupoteza sifa ya nchi,” alisisitiza.

Kozi za Waamuzi wa Mpira wa Miguu wa Tanzania ilianza Julai 25, 2016 ambako iliendeshwa na wakufunzi Carlos Henrique kutoka Afrika Kusini, Mark Mzengo kutoka Malawi na Felix Tangawarima wa Zimbabwe.

Leo Julai 29, 2016 limeanza darasa la waamuzi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara (VPL), Ligi Daraja la Kwanza ya StarTimes (FDL) na Ligi Daraja la Pili (SDL) kwa msimu wa 2016/2017.
mwisho

MAKONDA MGENI RASMI TAMASHA LA VIJANA-

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kesho Jumamosi Julai 30, 2016 anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye uzinduzi wa mashindano ya kuibua na kukuza vipaji vya mpira wa miguu kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume ulioko kwenye makutano ya Barabara za Uhuru na Shaurimoyo, Ilala jijini Dar es Salaam.

Sambamba na Makonda, Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi naye amethibitisha kuwako kwenye hafla hiyo ambayo mchezo wa kwanza utazikutanisha timu za Ilala Boys dhidi ya Bombom Ilala, Dar es Salaam. Inawakilishwa na mikoa yote mitatu kisoka ambayo ni Ilala, Kinondoni na Temeke kwa pande zote mbili za wavulana na wasichana.

 Kadhalika, wakuu wa mikoa mingine ambayo mashindano hayo yatafanyika nao watakuwa wageni rasmi katika mikoa yao ambayo ni Mbeya, Mwanza na Morogoro kwa upande wa wavulana pia Arusha, Lindi na Zanzibar kwa upande wa wasichana.


MALINZI ATOA SALAAM ZA RAMBIRAMBI KWA MSIBA WA SANGA

RA
IS wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amemtumia salamu za rambirambi Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri (TEF), Theophil Makunga kutokana na kifo cha Joseph Senga – Mpigapicha Mkuu wa Gazeti la Tanzania Daima.

Rais Malinzi amepokea taarifa za kifo cha mwandishi huyo mwandamizi wa habari aliyebobea kuripoti habari za aina mbalimbali ikiwamo za michezo nchini kilichotokea jioni ya Julai 27, 2016 huko India, alikokuwa akipatiwa matibabu ambako habari za kifo chake zilianza kusambaa usiku wa kuamkia jana Julai 28, 2016 kabla ya kuthibitishwa na Mhariri Mtendaji wa Free Media, Neville Meena.

 Salamu za rambirambi za Rais wa TFF Malinzi pia zimekwenda kwa familia ya marehemu Joseph Senga, ndugu, jamaa na marafiki na kuwataka kuwa na moyo wa subira wakati huu mgumu wa msiba wa mpendwa wao.

Malinzi alimwelezea Joseph Senga, wakati wa uhai wake alikuwa na mchango mkubwa katika tasnia ya habari za michezo akitoa mawazo yake hivyo ameacha alama ya ucheshi, kujituma na uwajibikaji katika kufanikisha kazi zake katika gazeti la Tanzania Daima na wakati fulani magazeti ya Kampuni ya New Habari House 2006.

Mwenyezi Mungu aipumzishe roho ya marehemu Joseph Senga mahala pema peponi.

MO KUWEKA SIMBA BILIONI 20



Abdallah Moghamed

MFANYABIASHARA Mohammed Dewji 'MO' amejitokeza hadharani na kukiri yupo tayari kufanya uwekezaji wa bilioni 20 kwa klabu ya Simba endapo wanachama wa klabu hiyo wataridhia.

Mo amekuwa akihusishwa na kutaka kufanya uwekezaji huo mkubwa ndani ya Simba huku baadhi ya wanachama wa klabu hiyo wakionekana kutokuwa tayari kutokana na sababu zao binafsi.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisi kwake jijini Dar es Salaam MO alisema kinachomvutia kufanya uwekezaji huo mkubwa kwa Simba ni mapenzi aliyonayo kwa klabu hiyo huku akijaaliwa kipato kikubwa na Mungu.

"Simba naipenda toka moyoni, niliwahi kuidhamini miaka ya nyuma na tulifanya vizuri sana katika michuano ya kimataifa kila mwanasimba analijua," alisema MO.

Aidha Mo alisema bajeti ndogo ya Simba ndiyo inayoifanya klabu hiyo kushindwa kushindana katika solo la usajili na kutowalipa vizuri wachezaji kama ilivyo kwa Yanga na Azam.

Wakati huo huo MO alisema ndani ya miaka mitatu endapo atakubaliwa  kufanya uwekezaji atajenga kiwanja bora cha mpira, hosteli, Gym na kuajiri kocha mwenye vigezo.

Simba inatarajiwa kufanya mkutano mkuu wa wanachama utakaojadili juu ya uwendeshwaji wa klabu hiyo siku ya Jumapili katika Bwalo la maofisa wa Polisi Oysterbay.
........................

TAMASHA LA WANYASA DAR ES SALAAM

Karibuni kijiji cha Makumbusho kuanzia leo,  kesho na jumapili katika Tamasha la Wanyasa,  mtaweza kufahamu historia yetu,  vyakula vyetu vya asili,  mavazi yetu ya asili,  ngoma zetu za asili utakuwepo Mganda nk,  pia unawezajipatia unga fresh wa muhogo,  kisamvu,  dagaa wa Nyasa,  samaki,  Likungu kwa bei nafuu,  Mkataa kwao Ni Mtumwa,  Najivunia Ruvuma Yangu,  najivunia Nyasa yangu.

TCHETCHE AZIKANA SIMBA,YANGA

MBULIAJI wa Azam FC, Kipre Tchetche amesema hajawahi kufanya mazungumzo na klabu kongwe hapa nchini za Simba na Yanga kwa ajili ya kuzitumikia timu hizo kwa msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Kipre ambaye yuko nchini kwao na huku pacha wake Michael Bolou tayari amejiunga na kikosi cha timu hiyo kinachojiandaa na Ligi hiyo pamoja na michuano ya kimataifa (CAF) mwakani.
Kuna tetesi kwamba mchezaji huyo amegoma kurejea nchini huku akihitaji uongozi wa Azam kumruhusu ili ajiunge na mmoja ya timu hizo mbili Simba au Yanga.
Akizungumzia sakata hilo, Kipre aliyekuwa nchi kwao Ivory Coast, alisema hana mpango wa kucheza soka Tanzania hivyo hakuna ukweli  suala la kufanya mazungumzo Simba au Yanga.
Alisema hayo maneno amekuwa akizushiwa tangu msimu uliopita ambapo walianza kumuhusisha na Yanga ambapo kwa sasa Simba jambo ambalo halinaukweli.
“Hayo maneno sio ya kweli kabisa kwa sasa sijafikiria kucheza soka Tanzania, nahitaji kupata changamoto za soka nchi zingine mbali na Tanzania kwani nimekaa na kucheza soka zaidi ya miaka mitatu ,” alisema.
Kipre ambaye bado yuko nchini kwao licha ya pacha wake Michael Boluo kujiunga na timu hiyo iiliyopo kambini kwa ajili ya maandalizi ya Ligi Kuu pamoja na michuano ya kimataifa (CAF) mwakani.
Alisema hadi sasa hajakuwa na maamuzi sahihi zaidi ya kuisubiri viongozi wake kuweza kumpa ruhusa hiyo ya kumuondoa katika kikosi chao kwa msimu ujao.
“Suala la lini nitakuja huko bado sijajua kwani viongozi hawajaonyesha nia yoyote ya kuniondoa jina langu katika orodha ya wachezaji wao msimu ujao, hivyo ka

UCHAGUZI BFA WASIMAMISHWA


Na Tausi Salum 

KAMATI ya Uchaguzi ya Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Pwani (COREFA), kwa mara nyingine imeusimamisha uchaguzi wa Chama cha Soka Wilaya ya Bagamoyo (BFA) uliokuwa ufanyike kesho July 30, 2016.

Mwenyekiti Kamati ya Uchaguzi Mkoa wa Pwani (COREFA),Masau Bwire  kuwa kusimamishwa kwa uchaguzi huo ni kutokana na mapingamizi kutoka kwa baadhi ya wagombea wakipinga mfumo mzima wa usaili uliofanyika jana na kuwahalalisha wagombea wote kuingia katika kinyang'anyilo wakati miongoni mwao wakiwa hawana sifa za kuwa wagombea.

Alisema kuwa Hussein Kipindula ni mmoja wa wagombea anayeomba kugombea nafasi ya Katibu wa BFA ambaye amewasilisha katika Kamati yangu pingamizi la kupinga baadhi ya wagombea kuruhusiwa kugombea nafasi walizoziomba wakati hawana sifa.

Bwire alisema Katiba ya BFA ibara ya 29 (2) inaeleza sifa ya Elimu ya kuanzia kidato cha nne anayotakiwa kuwanayo yeyote anayetaka kugombea na kuchaguliwa kuwa kiongozi wa BFA, sifa ambayo Bw. Kipindula amesema wagombea baadhi hawana lakini wameruhusiwa kugombea!

Alisema kuwa Ili kuondoa mkanganyiko huo, Kamati yangu imeamua kuusimamisha uchaguzi huo, ili usaili uanze upya na kuiagiza Kamati ya Uchaguzi ya Wilaya ya Bagamoyo (BFA) kuleta kwa Kamati yangu nakala ya vyeti vya elimu vya wagombea vikaakikiwe Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA).

Ni matumaini yangu kwamba, maelekezo na maagizo ya Kamati yangu kwa Kamati ya Uchaguzi Bagamoyo (BFA) yatatekelezwa kwa haraka ili BFA iwapate viongozi wenye sifa kwa mjibu wa Katiba na Kanuni za uchaguzi za TFF na wagombea wote watatoa ushirikiano wa kutosha katika kuondoa mkanganyiko huo.



Wednesday, July 27, 2016

MWAKALEBELA CUP KUANZA SIKU ZA USONI

DIWANI wa Kata ya Wazo,  Mh .Joel Mwakalebela  amezitaka timu zote zilizopo katika Kata yake kujitokeza kwa wingi kuweza kushiriki katika mashindano ya Mwakalebela CUP yanayotarajiwa kuanza mwezi wa Septemba.

Akizungumza jana  Joel Mwakalebela alisema kuwa mitaa nane itashirikia katika mashindano hayon na  lengo  ya kuanzisha mashindano hayo ni  kwaajili ya kusaka vipaji na kukuza soka.

"Vijana wengi wanavipaji ila wanakosa wadhamini wa kuwaendeleza katika soka hivyo nimeamua kuanzisha mashindano hayo kwa lengo la kusaka vipaji kwa  vijana, kama tunavyojua soka ni  ajira naomba vijana kujitokeza kwa ajili ya kushiriki katika mashindano haya ili kupata timu bora katika Kata yangu"alisema.

Aliongeza kuwa katika mashindano hayo yatasimamiwa pia na mtaalam wa soka ambae ataangalia vipaji vya soka ili kuweza kupata vipaji vya soka katika Kata ya Wazo.

Alifafanua kuwa mashindano hayo yanatarajia kutoa timu moja kwa ajili ya Kata ya Wazo ambayo itashiriki katika mashindano ya soka na kuwakilisha kata ya wazo.



Tuesday, July 26, 2016

SERENGETI BOYS KAMBINI MADAGASSAR


 

 
Na Tausi Salum
DUAza Watanzania zielekezwe pia kwa timu ya Taifa ya Mpira 

wa Miguu ya vijana wenye umri wa chini ya miaka 17 ‘Serengeti 

Boys’, iliyoondoka leo saa 12.00 Uwanja wa Ndege ya Mwalimu 

Julius K. Nyerere, Dar es Salaam, Tanzania kwenda Antananarivo, 

Madagascar kupitia Uwanja wa Ndege wa Ndege ya Oliver Tambo 

jijini Johannesburg, Afrika Kusini.

Ofisa Habari wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) 

Alfred Lucas, alisema Serengeti Boys inayokwenda kuweka kambi 

huko Antananarivo, Madagascar inatarajiwa kufika huko saa 8.10 

mchana. Timu hiyo inajiandaa kucheza na Afrika Kusini katika 

mchezo wa awali kuwania nafasi ya kucheza fainali za Kombe la 

Mataifa ya Afrika utakaofanyika Agosti 6, 2016.

Alisema mchezo wa marudiano utafanyika Agosti 21, mwaka huu 

kwenye Uwanja wa Azam, ulioko Chamazi-Mbagala, nje kidogo ya 

jiji la Dar es Salaam. Serengeti ipo kwenye ushindani wa kuwania 

nafasi ya kufuzu fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa vijana, 

zitakazofanyika mwakani huko Madagascar.

Wakati mkuu wa msafara akiwa ni Ayoub Shaibu Nyenzi ambaye 

ni Mwenyekiti wa Kamati ya Soka la Vijana, maofisa wengine 

waliosafiri na timu hiyo ni Kocha Mkuu, Bakari Nyundo Shime, 

Daktari wa timu hiyo, Shecky Francis Mngazija na Mtunza Vifaa, 

Andrew Vanance Andrew pamoja na Juma Kaseja Juma ambaye 

kwa muda amechukua nafasi ya makocha wasaidizi, Sebastian 

Nkoma na Muharam Mohammed ‘Shilton’ wanaohudhuria kozi ya 

makocha ngazi ya juu inayoratibiwa na CAF.

Nyota waliosafiri ni pamoja na makipa, Ramadhani Awm Kabwili,

Kelvin Deogratius Kayego na Samwel Edward Brazio wakati 

mabeki wako Kibwana Ally Shomari, Nickson Clement Kibabage, 

Israel Patrick Mwenda, Dickson Nickson Job, Ally Hussein 

Msengi, Issa Abdi Makamba na Enrick Vitalis Nkosi.

Viungo ni Kelvin Nashon Naftal, Ally Hamisi Ng’anzi, Asadi Ali 

Juma Ali, Syprian Benedictor Mtesigwa, Ibrahim Abdallah Ali, 

Shaban Zuberi Ada huku washambuliaji wakiwa ni Mohammed 

Abdallah Rashid, Yohana Oscar Mkomola na Muhsin Malima 

Makame.

“Najua mchezo utakuwa mgumu, lakini nakiamini kikosi change. 

Kiko imara,” amesema Shime, maarufu zaidi kwa jina la Mchawi 

Mweusi.

Serengeti Boys inakwenda kucheza na Afrika Kusini baada ya 

kuwatoa Shelisheli kwa jumla ya mabao 9-0 katika mechi zake 

mbili za kimataifa. Mshindi wa jumla kati ya Serengeti Boys na 

Afrika Kusini, atacheza na timu mshindi kati ya Namibia na 

Congo-Brazaville.

 Hivi karibuni Serengeti Boys ilifanya ziara India ambako 

walishiriki mashindano ya vijana ya Kimataifa yanayotambuliwa na 

FIFA (AIFF International Youth Tournament 2016) kabla ya 

kurudi na rekodi ya kupigiwa mfano si tu katika Tanzania na kwa 

nchi za Afrika Mashariki. Ilishika nafasi ya tutu nyuma ya Korea 

Kusini na Marekani.
mwisho
 
 

Monday, July 25, 2016

Simba ni kombinesheni na mbinu kwa kwenda mbele

                                      

KOCHA Mkuu wa Joseph Omog akiendelea na programu ya kutengeneza kombinesheni, amepanga kuanza na programu ya mazoezi ya kimbinu kwa wachezaji wake ikiwa ni kuimarisha zaidi timu hiyo.

 

Simba wameweka kambi mjini Morogoro  ikiendelea na Program kwa ajili ya maandalizi ya msimu  ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara, utakaoanza Agosti 20.

 

Omog  amekuwa makini na program yake huku akihakikisha anatengeneza kombinesheni kwa wachezaji wake wapya ili kuendana na waliowakutana katika kikosi hicho.

 

Mcameroon huyo anaendelea na programu hizo huku akiwa na baadhi ya nyota wapya waliowasajili kwa ajili ya msimu ujao  ni Shiza Kichuya, Mohamed Ibrahim, Mzamiru Yassin na Hamad Juma.

 

Licha ya hayo pia kuna wachezaji wanne wako katika mchujo ambao ni Wakongo, Janvier Bokungu, Moussa Ndusha, Muivory coast, Blagnon Fredric na Mzimbabwe, Method Mwanjali.

 

Kocha huyo alisema  hivi sasa amezielekeza nguvu zake huko kwa kuhakikisha wachezaji wake wanashika mbinu mbalimbali anazowapa,

anataka kuona timu inacheza soka la pasi za haraka wakati timu ikiwa ina mpira ikishambulia kwenye goli la wapinzani.

 

Alisema yuko makini wakati timu inapopoteza mpira, lakini kwa pamoja wote wanatakiwa kukaba kwa kuanzia washambuliaji, viungo na mabeki.

 

“Baada ya kufanya kazi yangu ya awali ikiwemo Program ya kuwaweka wachezaji wangu kuwa fiti, ninahakikisha kutengeneza kombinesheni kwa wachezaji wake kabla ya Ligi,” alisema .

 

Alisema anahitaji kuona wachezaji wake wanacheza soka la pasi za haraka , kwa kushambulia kwa timu mpinzani pamoja na kukaba pia wasipoteze mpira.

 

 

YANGA IMEENDELEA NA MAZOEZI

YANGA imeendelea na mazoezi Leo usiku  imefanya mazoezi kwenye Uwanja wa shule ya Bohar mjini hapa kujiandaa na mchezo wa  Kesho dhidi ya wenyeji, Medeama ya Ghana.

Timu iliyowasili Ghana tayari kwa mchezo hao huo ambao utapigwa katika  Kesho , timu hiyo imepania kushinda mechi hiyo kufufua matumaini ya kwenda Nusu Fainali.

Yanga iliyondoka bila ya wachezaji wao watatu wakiwemo beki Mtogo  Vincent Bossou abaye ameeachwa Dar es Salaam,  anatumikia adhabu ya kadi mbili za njano, wengine wakiwa ni viungo Geoffrey Mwashiuya na Deus Kaseke ambao ni majeruhi.

Kocha Mkuu wa Yanga Mholanzi, Hans van der Pluijm amesema pengo la Bossou litazibwa na Nahodha Nadir Haroub ‘Cannavaro’ ambaye yuko fiti na kuicheza mchezo huo.

Amesema amefanyia kazi mapungufu yaliyojitokeza katika michezo iliyopita ambapo kazi yake amemaliza jijini Dar es Salaam, kazi iliyobakia ni vijana wake kufanya kazi.

“Kuna viungo wa kutosha, sifurahii kuwakosa Kaseke na Mwashiuya, lakini kwa kuwa hawapo kwa sababau ambazo zipo nje ya uwezo wetu, wengine watacheza badala yao,”amesema .

Kocha huyo amesema baada ya kumaliza kazi yake, hivyo anachokifanya ni kutoa maelekezo kwa wachezaji wake na kuhitaji vijana wake kushambulia na kuzuia.

Mazembe inaongoza Kundi A kwa pointi zake saba, ikifuatiwa na MO Bejaia pointi tano, Medeama pointi mbili, wakati Yanga yenye pointi moja inashika mkia.

 

 

Sunday, July 24, 2016

BALOZI WA TANZANIA INCHINI INDIA AMTEMBELEA HAJI MANARA HOSPITALINI


Balozi wa Tanzania nchini India, Mohammed Hija Mohammed leo amefika kumtembelea Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano cha Simba, Haji Manara.

Mohammed amemtembelea Manara katika hospitali ya Artemis jijini New Delhi akiwa ameongozana na Ofisa Mwandamizi wa Ubalozi huo, Yahya Mhata ambae pia alipata kuwa mwenyekiti wa FAT (TFF) miaka ya 2003/2004.

Manara yuko nchini India akipata matibabu ya macho yake baada ya jicho la kushoto kupoteza uwezo wa kuona huku lile la kulia likiwa limepuguza kabisa uwezo

OMOG AZUIA ZA KIRAFIKI SIMBA SC

Kocha mkuu wa Simba Joseph Omog ametangaza kuahirisha kwanza mechi za kirafiki ambazo zilitarajia kuanza kuchezwa jana, lakini sasa muda wake atautumia kwa mambo mawili.

Kwanza ni kuona wachezaji wengine ambao wamejiunga na kikosi chake, lakini ataanza na kupanga mikakati mipya baada ya kukiona kikosi chake.

Taarifa zinaeleza, leo pia wachezaji wa Simba wanapumzishwa na kocha huyo atakuwa muda mwingi na msaidizi wake, Jackson Mayanga wakipanga mambo kadhaa muhimu.

Habari za ndani ya kambi ya Simba, zimeeleza kuwa kila kitu kimekwenda kwa mpangilio waliotaka.

“Ndiyo maana kocha anachotaka ni kuhakikisha tutakapoanza mechi za kirafiki, basi moja kwa moja anakuwa anmalizia tu,” kilieleza chanzo.

Awali, Omog aliomba mechi tatu na tayari uongozi ulimtafutia dhidi ya Burkina Faso ya Morogoro mechi mbili, pia dhidi ya Polisi Moro.

ULIMWENGU KUWAKOSA MO BEJAIA

Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania anayechezea klabu ya TP Mazembe ya nchini Kongo, anatarajiwa kukosa mchezo Wa  Marejeano dhidi ya Mo Bejaia...

Ulimwengu maarufu Kama Rambo nchini Congo ataukosa mchezo huo baada ya kupata majeraha kwenye mguu wake wa kushoto.

Ikumbukwe kuwa, mechi ya mwisho iliyopigwa baina ya miamba hiyo ilishuhudia sare  ya 1-1 kabla  ya mchezo
huo utakaopigwa katikati ya wiki hii

AME ALI KUTUA SIMBA

Mshambuliaji wa Azam Fc Ame  Ali, huenda akajiunga rasmi na Simba Sc baada ya mazungunzo baina ya klabu hizo kwenda vizuri.

Akiongea na mtandao huu, mmoja wa mabosi wa  Simba Sc ambaye hakutaka jina lake litajwe, amesema Kuwa usajili huo unatarajiwa kukamilika ndani ya sana 48 zijazo.

Simba imejichimbia mkoani Morogoro tayari kabisa kwa kuanza kwa msimu wa 2016/2017 huku ikikabiliwa na shinikizo la kukosa nafasi ya kuiwakilisha nchi kwa muda wa  miaka minne  mfululizo.

PLUIJIM AJAKATA TAMAA KWA MEDEAMA

Tausi Salum

KOCHA Mkuu wa klabu ya Yanga, Hans van der Pluijm, amesema katika maisha ya soka ajakata tamaa, hivyo katika mchezo wao ujao dhidi ya Medeama lolote linaweza kutokea.

Akizungumza katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Pluijm alisema kuwa wako vizuri kwa ajili ya chochote kilichotokea, inawezekana ikatokea kilichotokea hapa nchini au kukawa na mabadiliko kwa klabu yake kupata ushindi.

Pluijm alisema katika mpira lolote linaweza kupatikana kwa kuwa wamejipanga kuvanya vizuri kikosi chake kina hali kubwa ya ushindi, hivyo kupata kwake ushindi katika mchezo huo ujao ni muhimu na wanautarajia kwa sababu wamejipanga vizuri.

"Katika maisha ya soka uwa sikati tamaa  nina amini kila jambo linaweza kutokea, matokeo kama yaliyotokea haoa nchini au tukashinda, maana hata kupata matokeo ya 1-1 kama ya hapa kwetu ugenini ni nafasi nzuri, lakini kushinda nako ni muhimu zaidi"alisema Pluijm.

Kikosi cha Yanga kimeondoka majira ya saa 10, usiku wa kuamkia leo kwa ajili ya mchezo wao wa Kombe la Shirikisho Barani Afrika dhidi ya Medeama.

Yanga imeondoka ikiwa chini ya Mkuu wa Msafara Hussein Nyika ambaye ni pia ni Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya klabu hiyo.

Mchezo kati ya Medeama dhidi ya Yanga utachezwa kwenye uwanja wa Essipong Sports uliopo kwenye mji wa Sekondi, Ghana. Mechi hiyo itakuwa chini ya mwamuzi wa kati Redouane Jiyed atakayesaidiwa na Mohamed Lahmidi na Hicham Ait Abboou.

Yanga itaingia uwanjani kupambana na Medeama ikiwa na kumbukumbu ya kutoka sare kwenye mchezo wa awali ilitoka sare ya kufungana goli 1-1 na kujiweka kwenye mazingira ya kusonga mbele kwenye hatua ya nusu fainali ya mashindano hayo.

Klabu hiyo ya mtaa wa Twiga na Jangwani, ipo nafasi ya mwisho kwenye Kundi A ikiwa na pointi moja.

Saturday, July 23, 2016

SIKINDE KUBURUDISHA MADALE LEO

Wadau wa maendeleo ya kijiji cha Madale Leo watapata burudani kabambe itakayotolewa na bendi maarufu Tanzania Sikinde katika ukumbi was kisasa kabisa Lemon barbeque ambao upon Jirani na kituo cha mabasi-magaigwa
Lengo mahsusi la burudani hiyo iliyoandaliwa na kundi maarufu na lenye nguvu ya ushawishi Wadau wa madale ni kuchangisha pesa kwaajiri ya kukamilisha ujenzi wa kituo cha polis Madale..kituo ambacho kwa asilimia 100 kimejengwa kwa nguvu  ya wananchi wa Madale hususani WADAU.
Wananchi wote mnakaribishwa
Kwa kushiriki ktk burudani hiyo utakuwa umechangia katika ujenzi wa kituo cha polis kupitia malipo yako ya kiingilio

Thursday, July 21, 2016

MANARA APATA AHUENI INDIA

matumaini kwa Haji Manara atarejea na kuona kama kawaida baada ya matibabu yake jijini New Delhi nchini India.

Manara amezungumza na mtandao leo na kusema tayari ameanza vipimo na ana matumaini.

"Nimemaliza vpimo vya awali na kuonyesha matumaini ya kupona. Tayari nishaanza tiba na kesho natarajiwa kulazwa hospitali kwa siku tatu kwa uchunguzi zaid na matibabu.   

"Imani imekuwa kubwa kwa majibu ya leo, ambayo yanaonyesha kuvilia na kuganda kwa damu katika macho yangu.                            

"Madaktari wanasema upo uwezekano mkubwa wa kupona ila watajua zaidi baada ya kumaliza tiba ya awali na uchunguzi," alisema Manara.

Manara amesafirishwa kwenda India baada ya kuamka asubuhi jicho lake likiwa halioni kabisa huku moja likiwa limepoteza uwezo na kubaki kwa asilimia 10 tu.

MWASHIUYA NJE MIEZI MITATU

Kiungo kinda wa Yanga, Geofrey Mwashiuya amepata msala mwingine baada ya vipimo vya MRI kuonyesha ana ana tatizo la goti linalomlazimu kukaa nje ya uwanja kwa mwezi mmoja na nusu.

Mwashiuya tayari ameanza kufanyiwa matibabu jijini Dar es Salaam chini ya usimamizi wa daktari wa Yanga.

Kukaa kwake nje, kutamlazimu kuzikosa mechi tano hadi kumi za mwanzo za Ligi Kuu Bara ambayo itaanza rasmi Agosti 20.

Taarifa zinaelezwa, Mwashiuya amewekewa bandeji laini ambayo inamsaidia kupona haraka na imeelezwa aina hiyo ya bandeji ni kama ile aliyofungwa mshambuliaji wa Leicester City, Jamie Vardy

MAVUGO KUFANYA MAJARIBIO UFARANSA

Laudity Mavungo huenda ikaota mbao baada ya juzi kukutwa uwanja wa ndege wa nchi burundi kwenda nchini Ufaransa kwa ajili ya majaribio katika klabu ya Tours inayoshiriki ligi daraja la pili.

Simba ambayo iliingia mkataba na straika huyo mwaka jana ambapo alikuwa na mkataba wa mwaka mmoja na vital'O iliyohitaji dau kubwa ili kumuachia mchezaji huyo kujiunga Simba.

Taarifa za uhakika zilizoifikia jijini jana kutoka kwa rafiki wa karibu wa Mavugo kwamba mchezaji huyo amepata dili Ufaransa na juzi (jumamosi) kwenda nchini humo kwa majaribio.

Alisema siku hiyo alikutana na mchezaji huyo uwanja wa ndege akiwa na familia yake ikimuaga kwa ajili ya safari ya kuelekea nchini humo.

"Nilikutana nae uwanja wa ndege wa Burundi, akiwa na familia yake wakimuanga kwani amepata ofa ya kwenda ufransa kufanya majaribio katika timu ya Tours inayoshiriki ligi daraja la pili," alisema rafiki huyo.

Alisema endapo Mavugo akifuzu katika majaribio hayo huenda asijiunge tena na Simba wala Vital' O na kusaini mkataba katika timu hiyo.
@@@@@

PLUIJM AITEGA MEDEAMA

KOCHA wa timu ya Yanga Mholanzi Hans Van Pluijm hajakata tamaa na naona kuna uwezekano mkubwa wa kikosi chake kusonga mbele katika hatua ya nusu fainali ya kombe la shirikisho barani Afrika.

Yanga ipo katika hatua ya makundi ya kombe la shirikisho jana aliamvulia pointi 1 katika michezo aliyocheza ambapo jana alilazimishwa sare ya bao 1-1, mchezo uliochezwa uwanja wa taifa.

 Mabingwa hao wa ligi kuu Tanzania bara hawana nafasi baada ya kijikusanyia alama moja huku wakiwa na michezo miwili ugenini na mmoja nyumbani dhidi ya Mo Bejaia ambao waliwafunga katika mchezo wa awali.

Pluijm alisema vijana wake walicheza vizuri lakini tatizo la kutokutumia nafasi wanazopata linaendelea kuwaandama.

"Tunaweza kufuzu katika hatua ya nusu fainali , kwakua katika mpira kila kitu kinawezekana,tumebakiwa na mechi tatu na tukishinda zote tutakuwa na alama kumi," alisema.

Hans alisema hajakata tamaa akiamini mechi zilizobakia ikiwa moja ya nyumbani na ugenini kufanikiwa kushinda.

Alisema baada ya mchezo wao dhidi ya medeama wanaenda kufanyia kazi mapungufu yaliyojitokeza katika mchezo huo na kujiimarisha katika michezo iliyobakia ya kundi hilo.